Mobetto Athibitisha Kutolewa Posa ya Shilingi Milioni 10
HAMISA Hassan Mobetto au Misa; ni mwanamitindo, msanii wa muziki na mjasiriamali maarufu Bongo ambaye anafunguka kuwa, aliwahi kutolewa posa mara nyingi na posa ndogo ilikuwa ni shilingi milioni 10.
Hamisa amesema; “Nilishawahi kutolewa posa mara nyingi sana na wengine siwafahamu na wengine nawafahamu, lakini unakuta mambo hayajakaa sawa maana suala la ndoa ni la kujipanga.
“Posa ndogo ambayo ilishawahi kuja nyumbani ilikuwa million kumi.
Mimi nina watoto na nimekuwa kwenye mazingira ya kushuhudia baadhi ya ndugu zangu wananyanyasika sababu hawana chao hivyo kabla sijaingia kwenye ndoa nataka nijikamilishe ili hata nikiingia niwe full na hata miaka ya mbele ikishindikana basi niwe na vyangu…”
Hamisa ni mama wa watoto wawili, mmoja amezaa na Mkurugenzi wa EFM na ETV, Majizzo na mwingine amezaa na staa wa muziki wa Kimataifa nchini Tanzania, Diamond Platnumz.
Cc; @sifaelpaul