Moto Wateketeza Maduka Zaidi ya 10 Kagera
MOTO umeunguza maduka zaidi ya 10 na kuteketeza baadhi ya vitu katika majengo yanayomilikiwa na familia ya Nekemia Kazimoto yaliyopo Mji wa kayanga mjini, Karagwe, Kagera mkabala na majengo ya city center na Magereza ya kayanga
Mkuu wa Wilaya ya Karagwe Godfrey Mheluka aliongoza wananchi kuzima moto huo ambao uliibuka saa 5 na dakika 20 usiku Desemba 26 katika moja ya duka la nguo na kusambaa katika maduka mengine ya bidhaa za vyakula, hoteli, stoo za vifaa vya ujenzi, salooni na maduka ya bidhaa mchanganyiko.
Mheluka amesema kuwa chanzo cha moto huo hakijafahamika mpaka sasa.
Mheluka amesema kuwa chanzo cha moto huo hakijafahamika mpaka sasa.