The House of Favourite Newspapers

Mr Championi Kugawa Zawadi Leo

shinda-nyumba-17

MWANDISHI WETU | CHAMPIONI, Dar es Salaam

WAKATI mamia ya wasomaji wa magazeti ya Glo­bal Publishers wakiende­lea kujaza kuponi kwa aji­li ya shindano la awamu ya pili ya Shinda Nyumba, leo Jumatatu Mr Champi­oni atakuwa mitaani jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kugawa zawadi kwa wa­somaji hao.

shinda-nyumba-2Ofisa Masoko wa Global Publishers, Jimmy Haroub akimuelekeza msomaji namna ya kujaza kuponi ya Shinda Nyumba.

Kwa mujibu wa Meneja Mkuu wa Global Publish­ers, Abdallah Mrisho, Mr Championi atampatia zawadi msomaji yeyote atakayekutwa akijaza kupo­ni hiyo mahali popote.

“Hii ni sapraizi kwa wa­somaji wetu, Mr Championi atakuwa akikatiza katika mitaa mbalimbali jijini Dar na kumsapraizi yeyote atakayekutwa akijaza kuponi yake tayari kuituma kwetu, hatuwezi kusema tu­tatoa kitu gani, lakini ni kitu ambacho kitamfurahisha msomaji,” alisema Mrisho.

shinda-nyumba-20Mr. Uwazi akigawa zawadi ya kofia kwa msomaji ba mkazi wa Goba.

Alitumia nafasi hiyo ku­wataka wasomaji kujiweka tayari kupokea zawadi yao mara tu wakimuona Bwana Championi mitaani na kuwa wasisahau kujaza kuponi zao mara baada ya ku­nunua magazeti hayo am­bayo ni Championi, Uwazi, Risasi, Amani, Ijumaa na Ijumaa Wikienda.

Droo ya kwanza ndogo kwa ajili ya shindano hilo itachezeshwa Februari 8, mwaka huu na baada ya hapo, kila mwezi itafanyika droo nyingine ambapo za­wadi mbalimbali zitatolewa kwa washindi.

shinda-nyumba-17Katika tukio hilo la kwan­za, zawadi zitakazotolewa ni pamoja na pikipiki, tele­visheni, simu aina ya smart­phones na vyombo vya ndani.

Global Publishers juzi ili­wafikia wasomaji wake wa maeneo ya Msasani, Tan­dale, Magomeni, Mwanan­yamala, Sinza na kwingine­ko ambapo wamejitokeza kwa wingi kununua maga­zeti na kujaza kuponi kwa ajili ya kushinda nyumba awamu ya pili.

shinda-nyumba-13Msomaji akizawadiwa tisheti baada ya kununua gazeti la Uwazi.

“Nawakubali sana Glo­bal na mimi nimeamua ku­shiriki baada ya kugundua kuwa Shinda Nyumba ni ya ukweli baada ya kumuona mshindi kutoka mkoani Irin­ga akizungumza mwenyewe kuwa kashinda kwa ku­nunua magazeti yenu,” al­isema Yusuph wa Tandale.

Wakazi wa Goba ambao pia walitembelewa na timu ya Shinda Nyumba, nao walisema hawawezi kukaa kimya bila kupata kuponi za shindano hilo wakati kila mmoja hivi sasa ana­zungumzia kuhusu zawadi bwerere kutoka Global Pub­lishers.

shuinda-nyumba-1“Siyo lazima mtu ushinde nyumba maana hiyo ni zali la mentali kweli, lakini ja­mani hivi vitu kama simu na vyombo vya nyumbani uvikose? Mimi natamani sana simu ya tachi, nitajaza kuponi hadi nipate,” alise­ma Consolata Simon, ali­yekutwa kijiweni kwake kwa mama ntilie, huko Goba.

Msomaji mwingine Un­aris Yunus, wa Goba njia panda, alisema awamu ya kwanza ya Shinda Nyumba hakuweza kupata zawadi yoyote, lakini safari hii moyo wake unamsukuma kuamini atakuwa miongoni mwa washindi.

shinda-nyumba-19Msomaji akizawadiwa tisheti ya Shinda Nyumba

“Kwanza nasikia zawadi zimeongezeka, sasa kama mnavyosema pikipiki itatolewa kila mwezi, sasa nikose nyumba sawa, basi pikipiki, tel­evisheni, simu, mashu­ka, branketi hadi vyo­mbo vya ndani nikose? Aaah jamani, Mungu nisaidie,” alisema Yu­nus.

Meneja Mkuu wa Global Publishers, Ab­dallah Mrisho alizidi kuwasisitiza wasomaji kuhakikisha wanajipa­tia kuponi za kutosha tayari kwa droo ndogo ya kwanza ambayo ita­fanyika hiyo Februari 8, mwaka huu.

shinda-nyumba-12Msomaji akijaza kuponi ya Shinda Nyumba.

“Utaratibu wetu wa kutuma kuponi ni ul­eule, baada ya kununua gazeti letu lolote kati ya Championi, Risasi, Uwazi, Amani, Ijumaa na Ijumaa Wikienda, kata kuponi kisha jaza kwa kadiri ili­vyoelekezwa, halafu pe­leka kwa wakala yeyote al­iye jirani na wewe, maana mawakala wetu wapo nchi nzima, au kwa wale wa Dar es Salaam, wanaweza kuzi­leta katika ofisi zetu zilizo­po Bamaga, Mwenge jijini Dar,” alisema.

Kwa stori zote kali, Tucheki…

Facebook @Globalpublishers

Twitter @GlobalHabari

Instagram @GlobalPublishers

YouTube @GlobalTVTZ

Endelea kutembelea website ya Global Publishers kila siku, tutaendelea kukusogezea kila news inayotokea mahali popote duniani.

Save

Shinda Nyumba Awamu ya Pili Yatikisa Jiji la Dar es Salaam

Save

Comments are closed.