Waziri Jafo Akutana Na Naibu Katibu Mkuu Mndeme, Dodoma
Naibu Katibu Mkuu (Mazingira) Ofisi ya Makamu wa Rais Bi. Christina Mndeme amefika ofisini kwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), Dkt. Selemani Jafo kujitambulisha baada ya kuwasili rasmi Ofisi ya Makamu wa Rais katika Mji wa Serikali, Mtumba jijini Dodoma Machi 19, 2024.