The House of Favourite Newspapers

Nay: Fred Vunja Bei Mshamba wa Mademu, Tutamsahau

0

RAPA maarufu Bongo, Nay wa Mitego ameamua kumpiga dongo mfanyabiashara Fredy Vunjabei akidai kuwa ni mshamba wa mademu wa mjini hivyo muda si mrefu atafirisika na mademu watamkibia.

 

Hii imekuja ikiwa ni siku chache baada ya Fredy kusema kuwa mwanamme lazima amhonge pesa mpenzi wake, akiongeza kuwa ukiwa kwenye mahusiano ambayo hauombwi pesa basi ujue kuna tatizo pahala.

 

“Naomba mumkumbushe Fred kua walikuwepo wauza nguo kama yeye walikuwa na hela kuliko yeye, walikuwa washamba wa mademu wa mjini kama yeye na wakafilisika na hawapo tena, so na yeye kwa ushamba huo huo wa mademu tutamsahau ni muda tu #hawakatai zikiisha sasa,” ameandika Nay wa Mitego.

 

Leave A Reply