Nyumba Yateketea kwa Moto Magomeni Dar (Video)
Nyumba moja iliyopo Magomeni Makanya jijini Dar wanayoishi wanafamilia na wapangaji leo imeteketea kwa moto ambapo wenyewe wakidaiwa kuwa kwenye msiba Mbezi jijini. Taarifa zilizopatikana eneo la tukio zilidai kuwa nyumba hiyo ilianza kuonekana ikiungua kunako saa nne asubuhi chanzo chake kikidaiwa kuwa hitilafu ya umeme.
Mwandishi wetu akiwa eneo la tukio aliwakuta askari wa kikosi cha Zimamoto wakiendelea kuuzima moto huo huku askari polisi wenye silaha wakilinda usalama eneo hilo hasa kudhibiti vibaka.
HABARI/PICHA: RICHARD BUKOS / GPL