Pacha wa Ney wa Mitego Awa Gumzo Mtandaoni
Emmanuel Elibariki ‘Nay wa Mitego’.
Baada ya kuibuka msanii chipukizi wa Bongo Fleva anayefanana sana kwa sura na msanii kutoka WCB, Harmonize kiasi cha kubatizwa jina la ‘Pacha wa Harmonize’, Harmorapa, katika mitandao ya kijamii inasambaa picha ikimuonesha pacha wa msanii wa Bongo Fleva, Emmanuel Elibariki ‘Nay Wa Mitego’, aliyebandikwa jina la ‘Ney wa Mitego Rapa’.
Picha ya utani mtandaoni iliyofananishwa na Ney wa Mitego (kushoto) na (kulia) ni Emmanuel Elibariki ‘Nay Wa Mitego.
Mashabiki wa Ney wa Mitego hawajapendezwa na picha ya pacha wa Ney wa Mitego, japo ni utani mashabiki hao wamedai inamdhalilisha Ney true boy.
Mpaka muda huu Ney wa Mitego hajatoa tamko lolote juu ya picha hiyo ya pacha wake mtandaoni.
Emmanuel Elibariki ‘Nay Wa Mitego’.
Salum Milongo/GPL
Comments are closed.