The House of Favourite Newspapers

Picha: Mawaziri 5 Watembelea Mpaka wa Tanzania na Uganda – Kagera

0
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. William Lukuvi akiongea na Mkuu wa Wilaya ya Missenyi Luteni Kanali Denice Mwila kuhusu changamoto za mpaka huo wngine ni Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe. Suleman Jaffo, Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mhe. Hamad Masauni, Naibu Waziri wa Maji na Umwagiliaji Mhe. Mhandisi Isack Kamwelwe na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Suzan Kolimba.

 

Mawaziri watano wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania watembelea mpaka wa Tanzania na Uganda ili kutatua changamoto zinazoukabili mpaka huo na kuuboresha.

 

Jiwe la mpaka wa Tanzania na Uganda namba 30.

 

Mawaziri hao ni Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. William Lukuvi, Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mhe. Hamad Masauni, Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe. Suleman Jaffo, Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Suzan Kolimba na Naibu Waziri wa Maji na Umwagiliaji Mhe. Mhandisi Isack Kamwelwe.

 

Ujumbe wa Mawaziri kutoka Serikali ya Jamhuri ya Muungano Tanzania wakiwa juu ya Jiwe la mpaka wa Tanzania na Uganda namba 30.

 

Miongoni mwa maeneo yaliyotembelewa na Mawaziri hao ni eneo la mpaka ya Tanzania na Uganda kwa upande unapo pita mto Kagera na eneo la kivuko cha mpaka wa Tanzania na Uganda kilichopo Mtukula mkoani Kagera.

Moja ya jiwe la mpaka wa Tanzania na Uganda ambalo Mawaziri wamefanya ziara ya kuliona.

 

Katika ziara hii Mawaziri hao wameweza kujionea hali halisi ya maisha ya wakazi wa mipakani na jinsi wanavyohusiana na wenzao wa nchi ya jirani ya Uganda ambapo wamekuwa wakishirikiana na kuishi kwa amani katika shughuli zao za kila siku.

Ujumbe wa Mawaziri kutoka Serikali ya Jamhuri ya Muungano Tanzania wakipita katika eneo la kivuko cha mpaka wa Tanzania na Uganda kilichopo Mtukula mkoani Kagera.

Aidha, ziara hii ni maandalizi ya Mkutano wa ujirani mwema kati ya Mawaziri wa serikali ya Uganda na Mawaziri kutoka Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambao unatarajiwa kufanyika mnamo tarehe 29 Julai 2017, Bukoba mkoani Kagera.

Ujumbe wa Mawaziri kutoka Serikali ya Jamhuri ya Muungano Tanzania wakikagua huduma za vibali vya kuingia na kutoka nchini Tanzania na Uganda zilizopo Mtukula mkoani Kagera.

 

Eneo la mpaka ya Tanzania na Uganda kwa upande unapo pita mto Kagera.

 

Leave A Reply