Rais Magufuli Apima Corona Dodoma
RAIS John Magufuli leo amepima joto la mwili katika harakati za upimaji zinazoendelea nchini na duniani kote kugundua na kukabiliana na mambukizi ya homa ya virusi aina ya Corona.
Amefanya hivyo kabla ya kuingia katika ukumbi wa baraza la mawaziri kuongoza kikao cha baraza hilo hko Chamwino, Dodoma.
Kipimo hicho hutumika miongoni mwa vipimo vya awali ambavyo hutambua iwapo mtu ana dalili za virusi hivyo kabla kufanyiwa kipimo kikubwa.
Mkuu huyo wa nchi amefanya hivyo ikiwa pia ni sehemu ya kuwahamasisha wananchi kuchunguza afya zao na kuchukua tahadhari kuhusu ugonjwa huo hatari ambao umeua maelfu ya watu duniani kote.
Kikao hicho kimehudhuriwa na Makamu wa Rais, Samia Hassan; Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa; mawaziri wote, manaibu mawaziri na viongozi wakuu wa vyombo vya ulinzi na usalama.