Rais Samia Amteua Abdul-Razaq Badru kuwa Mkurugenzi PSSSF
Rais Samia Suluhu Hassan amemteua Abdul-Razaq Badru kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF), ambapo aliyekuwa Mkurugenzi Mkuu wa PSSSF, CPA Hosea Kashimba atapangiwa kazi nyingine
Kabla ya uteuzi huu Badru alikuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya juu (HESLB)