The House of Favourite Newspapers

Ripoti ya CAG Yatua Bungeni

0

Ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi wa Hesabu za Serikali (CAG) imewasili bungeni jijini Dodoma leo na Spika wa Bunge, Job Ndugai amesema ataikabidhi ripoti kwa kamati mbili za Bunge.

 

Akizungumza bungeni leo, Ndugai amesema ripoti hiyo ataikabidhi kwa Kamati ya Hesabu za Serikali (PAC) na Kamati ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC).

 

Ndugai ameyasema hayo muda mfupi baada ya Serikali kuwasilisha taarifa za ukaguzi wa hesabu za wizara, taasisi na mashirika yaliyo chini yao.

Waliowasilisha taarifa ni Wizara ya Tamisemi, Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano, Ofisi ya Waziri Mkuu, Wizara ya Ujenzi na Ofisi ya Rais Utumishi.

Leave A Reply