Riyama Awashambulia Wezi wa Akaunti za Mastaa
MSANII wa Bongo Muvi nchini Riyama Ally, ‘Riyama’, amewafungukia na kuwashambulia wezi wa mtandaoni wanaofanya hivyo kwa kutumia akaunti za watu maarufu.
Amesema wezi hao wameichukua akaunti ya mumewe na kufuta picha zote kisha kutangaza kuiuza kwa Sh. 70,000.
Aidha Riyama ameeleza kuwa mwizi huyo ameshapatikana na watamchukulia hatua za kisheria ili liwe fundisho kwa wezi na matapeli wengine wa mtandaoni.
Comments are closed.