Serikali imesema ipo katika mpango wa kupitia utaratibu wa malipo kwa wanufaika wa Mikopo ya Elimu ya Juu ili wapunguziwe mzigo.
Naibu Waziri wa #Elimu, Omari Kipanga, amesema hayo akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalum, Halima Mdee, aliyehoji ni lini Serikali itapeleka mapendekezo ya #Sheria ili kuwaondolea mzigo wanufaika wa Mikopo kwani mpango huo umekuwa Biashara.
Halima Mdee amesema, “Serikali inasema inawasaidia watoto wa masikini wakati inawaumiza kwa mlolongo wa madeni.”