The House of Favourite Newspapers

Sitti: chozi langu limenifidia

0

wiwSitti Mtemvu. 

Na Imelda Mtema
SITTI Mtemvu, mrembo aliyeshinda taji la Miss Tanzania Mwaka 2014 lakini akavuliwa baada ya kubainika udanganyifu, amesema chozi lake alilomwaga siku za nyuma, limem-faidisha kwani hivi sasa anaishi kwa amani na furaha.

Akizu-ngumza hivi karibuni jijini Dar, Sitti alisema alipata maumivu makali siku alipovuliwa taji hilo, lakini alijipa moyo huku akifarijiwa na watu wake wa karibu.

“Naamini kila chozi langu lililodondoka lina faida kubwa maana imenifanya nisimame upya tena nikiwa na nguvu mno huku nikifarijika na kazi ambayo naifanya katika jamii yangu,” alisema Sitti anayemiliki mfuko wa kijamii wa Sitti Foundation unaosaidia jamii ya wanaoishi katika mazingira magumu.

Leave A Reply