TANZIA: Mfalme T’Challa wa Black Panther Afariki Dunia
Muigizaji maarufu duniani CHADWICK BOSEMAN amefariki dunia akiwa na umri wa miaka 43 jijini Los Angeles nchini Marekani kwa matatizo ya saratani ya utumbo mpana. Chadwick alijipatia umaarufu mkubwa kwenye filamu ya “Black Panther” kutoka studio za Marvel akiigiza kama Mfalme T’Challa.