The House of Favourite Newspapers

Vifurushi 21 Msaada wa Jack Ma Havikufika Kenya

0

Naibu wa Waziri wa Uchukuzi wa Kenya, Chris Obure amefichua kuwa vifurushi 21 vilivyokuwa na vifaa vya matibabu vilivyotolewa na wakfu wa Jack Ma mwezi Machi kama msaada wa kukabiliana na Covid 19 haikufika Kenya.

 

Obure amesema hayo juzi Alhamisi mbele ya kamati ya bunge ya afya japo hakudokeza ni vifaa vya aina gani vilikuwa ndani ya vifurushi hivyo.

 

Aliongeza kuwa vifaa hivyo havikuwahi kuwawasili nchini kutoka Ethiopia ambako misaada ya Jack Ma katika eneo hilo ilitumwa kwa ajili ya kusambazwa katika nchi zingine.

 

Wizara ya uchukuzi iligundua kuwa vifurushi 21 havikuwepo baada ya kuthibitisha hilo katika stakabadhi za kuegesha kutoka China.‘’Binafsi niliongea na maafisa wakuu wa Wizara ya Afya na walinithibitishia kuwa wanafuatilia suala hilo,’’ alisema Obure.

 

Kumekuwa na madai kwamba misaada ya Covid-19, ikiwemo ile kutoka kwa Ma ilitumiwa vibaya au kutoweka katika njia za kutatanisha.

Leave A Reply