Viongozi wa dini mbalimbali nchini, leo wamekutana katika Ukumbi wa Hoteli ya Golden Tulip, Posta jijini Dar es Salaam kujadiliana kuhusu umuhimu wa kurejesha upya mchakato wa kupata katiba mpya inayopendekezwa, ambao ulisimama tangu mwaka 2015.
Katika mkutano huo, viongozi hao wamezungumzia mambo mbalimbali ikiwemo mambo yaliyosababisha mkwamo wa mchakato wa katiba mpya na juu ya historia ya mchakato wa katiba ilivyoanza na maana halisi ya katiba.