The House of Favourite Newspapers

Washindi Wa Mwagika Challenge Ya Kilimanjaro Lager Wamekula Shavu

0

Ile video ya wimbo mpya wa “Energy” wa G’Nako iliyokuwa inasubiriwa kwa hamu sasa iko hewani.

Katika video hii wale washindi wa Mwagika challenge; Iddi Kidungwa, Michael Mwalembe na Nasma Msangi wamekula shavu la kutosha.

Shindano la ‘Mwagika Challenge’ lilikuwa na lengo la kuwapa fursa vijana kuonesha vipaji vyao na liliungwa mkono na mastaa wa Bongo Flava kama Shettah na Shilole waliokuwa mstari wa mbele kuhimiza mashabiki kushiriki shindano hilo, ambao wao pia ni miongoni mwa wasanii wanaonekana kwenye video hiyo.

Tazama video na endelea kuburudika na Kili Lager na usiache kufuatilia kurasa za Kili Lager kuona safari ya washindi hawa kuanzia mwanzo hadi mwisho.

Leave A Reply