Yemi Alade Amuunga Mkono Vanessa Mdee
BAADA ya Vanessa Mdee, mwimbaji Yemi Alade anaongezeka kwenye orodha ya wasanii wa kike ambao wanakitupia lawama kiwanda cha muziki na biashara yake nzima.
Kwenye ukurasa wake wa twitter, Yemi Alade mwanamuziki wa Nigeria, ameandika: “Biashara ya muziki ni ngumu sana, hakuna mtu anayetaka kukufurahia hadi unapoanza kupata mafanikio. Ninaomba tutieni nguvu, si rahisi.”
Yemi Alade ni miongoni mwa waimbaji nyota wa kike barani Afrika.