Yvonne Nelson: Bila make up, viatu virefu najisikia vibaya!
DIVA wa filamu kutoka Ghollywood anayewashika Nollywood, Yvonne Nelson amefunguka kuwa huwa anajisikia vibaya sana pale anapotoka ‘out’ bila kuwa na ‘make up’ au viatu virefu.
Yvonne aliyazungumza hayo alipokuwa katika uzinduzi wa Filamu ya If Tomorrow Never Comes uliofanyika katika Hoteli ya Capital View pande za Koforidua, Ghana.
Alisema filamu zimebadilisha maisha yake kwa kiasi kikubwa hasa linapokuja suala la kujipamba.
“Huwa najisikia vibaya sana ninapokosa urembo kwenye uso wangu pamoja na viatu virefu,” alisema Yvonne.