The House of Favourite Newspapers

MSANDO AFUNGUKIA LIVE VIDEO YAKE NA GIGGY MONEY

0

MWANASHERIA maarufu nchini aliyekuwa Chama cha ACT Wazalendo na hivi karibuni akahamia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Albert Msando, kwa mara ya kwanza amefunguka LIVE kuhusu video yake akiwa na mwanamuziki na modo Gigy Money iliyosambaa kwenye mitandao ya kijamii mwezi Mei mwaka huu.

Video hiyo ilimuonyesha Msando na Gigy Money wakiwa ndani ya gari, huku Msando akipitisha mkono wake juu ya mwili wa Gigy, wakati huo Gigy Money akikata kiuno huku anacheza muziki.

Akifanya mahojiano leo  kwenye Kipindi cha Clouds 360 kinachorushwa kupitia Clouds TV, Msando amesema;

“Ile ni moja kati ya sehemu zilizonisaidia katika maisha yangu, ilinisaidia kujua jamii inanichukuliaje na nini inategemea kutoka kwangu. Video ile haikutengenezwa kwa sababu zozote, mimi sikuwa namfahamu Giggy.

“Tukio lile lilitokea wakati nimekunywa kilevi, sikuwa nikitambua kilichokuwa kinaendelea. Zaidi ameeleza kuwa video ile ni funzo kwa jamii nzima kuwa responsible hata kama hujakamatwa, usisubiri uwe ‘caught on camera’ ili uwajibike,” alisema Msando.

Hata hivyo, baada ya video hiyo kusambaa watu mbalimbali walionyesha kuchukizwa na wanavyomfahamu Mwanasheria Albert Msando mtu wanayemwona ana  heshima kubwa na umaarufu katika jamii,  ambapo aliomba msamaha kupitia ukurasa wake wa Instagram.

Matukio kama haya na mengine, Install App Yako ya Kijanja na Namba Moja Tanzania ya Global Publishers

Android ===>Google Play

iOS ===>Apple Store

Leave A Reply