The House of Favourite Newspapers

ESTER KIAMA AKWAA SKENDO MBAYA

0
Ester Kiama.

STAA wa filamu za Kibongo, Ester Kiama ameingia kwenye skendo mbaya baada ya baadhi ya wasanii wenzake kudai katika siku za karibuni amekuwa akijitenga na kuonyesha maringo tofauti na zamani.

 

Wakizungumza na Za Motomoto News huku wakiomba hifadhi ya majina yao, baadhi ya wasanii wa kike walisema msanii huyo anaringa na kujitenga kwani hata kwenye shughuli au matatizo ya wasanii wenzake haonekani kushirikiana nao jambo ambalo linawakera.

 

Baada ya kupata madai hayo, Ester alitafutwa na kupatikana ambapo alisema; “Nimesikia hayo madai kwamba ninaringa, sijui eti najisikia siku hizi, lakini siyo kweli kabisa, sema kuna vitu vinaniweka busy sana, hivyo nakosa hata muda wa kujichanganya na wasanii wenzangu.”

 

STORI: GLADNESS MALLYA| RISASI MCHANGANYIKO JUMATANO

VIDEO: Serikali Yaagiza Magazeti Yote Tanzania Kusajiliwa Upya Kabla ya Oktoba 15

Leave A Reply