The House of Favourite Newspapers

Gazetia la ‘Ijumaa’ Laanza Kumwaga Zawadi kwa Wasomaji

0
Mkuu wa Kitengo cha Masoko cha Global Publishers, Anthony Adam (kushoto) akimkabidhi fulana ya gazeti la Ijumaa msomaji wa gazti hilo wa eneo la Goba.

GAZETI  namba moja la habari za burudani na mastaa nchini la Ijumaa limekuja kivingine baada ya kuzindua promosheni yake mpya ya chemsha bongo ambayo itakuwa inawawezesha wasomaji kujinyakulia zawadi kibao ikiwemo mkwanja kila wiki.

Wasomaji wa gazeti la Ijumaa wakifurahia jambo kabla ya kukabidhiwa zawadi.

Timu ya Masoko ya Global Publishers imetua mtaani leo na kuzindua rasmi promosheni hiyo ambapo msomaji atakayenunua gazeti hilo linalouzwa mtaani kwa Tsh 1,000 tu na kujibu maswali yaliyopo kwenye ukurasa wa pili, atakuwa ameingia katika kinyang’anyiro hicho cha ushindi.

 Adam (kulia) akimkabidhi mwanadada fulana ya gazeti la Ijumaa ambaye ni msomaji wa gazeti hilo wa eneo la Mbezi.

Kampuni  ya Global Group kazi yake ni kuhakikisha inawajali wasomaji wake kwa kuwarudishia fadhila, ndiyo maana imekuwa ikiwaletea zawadi mbalimbali kupitia promosheni mbalimbali na bahati nasibu.

…Akimkabidhi  fulana ya gazeti la Ijumaa msomaji wa gazeti hilo wa eneo la Mbezi Luis jijini Dar es Salaam.

Katika kuhakikisha chemsha bongo hiyo inawafikia wasomaji wake, timu ya maofisa masoko wa Global Publishers wameendelea kuwahamasisha wasomaji kununua nakala za gazeti hilo na kujibu maswali yanayopatikana katika ukurasa wa pili.

Msomaji wa Gazeti la Ijumaa akilisoma baada ya kukabidhiwa fulana yenye jina la gazeti hilo.

“Ukinunua Gazeti la Ijumaa ukurasa wa pili utakutana na chemsha bongo ambayo itakuwezesha kujibu maswali ili kujishindia Tsh. 30,000 (elfu thelathini) na tisheti bomba kabisa,” amesema Anthony Adam, Mkuu wa Kitengo cha Masoko wakati akiwaelezea wasomaji.

Wasomaji wa Gazeti la Ijumaa wakijaza kadi maalum kwa ajili ya kushindania fulana ya Ijumaa.

Baada ya kuhamishia mitandaoni pekee magazeti mengine ya Udaku ya Global Publishers, Ijumaa ndiyo Gazeti pekee la Burudani nchini Tanzania linalopatikana mtaani kwa sasa ambalo limeboreshwa kuanzia stori, upambaji wa kurasa, makala, machombezo na hadithi za mtunzi mahiri, Eric Shigongo.

Ofisa Masoko wa Global Publishers, Songoro Bilal (kushoto) akimrudishia fedha aliyonunulia gazeti baada ya kumkuta akisoma gazeti la Ijumaa.

Aidha, Ijumaa limesheheni kolamu zote kali zilizokuwa kwenye magazeti mengine Udaku ili kukufanya usi-miss kitu hata kimoja cha udaku iwe ndani ama nje ya Tanzania.

Msomaji wa eneo la Mbezi Mwisho akionyesha tabasamu  baada ya kujishindia fulana ya Gazeti la Ijumaa.
Nunua Gazeti la Ijumaa kila Ijumaa linapokuwa mtaani ili upate uhondo, si hivyo tu bali pia utapata zawadi za kutosha.

NA DENIS MTIMA | GPL

Leave A Reply