The House of Favourite Newspapers

Harmonize azidi kujiweka kwa kajala!

0

 

KITENDO cha mkali wa Bongo Fleva, Rajabu Abdul ‘Harmonize’ au Harmo kuendelea kumpostiposti muigizaji Kajala Masanja kimeonesha jinsi gani muigizaji huyo anazidi kujiweka karibu na mrembo huyo, mama wa mtoto mmoja.

 

Harmo alianza kuibua mjadala juu ya watoto wa wazuri kutoka Bongo Muvi akiwema Kajala kabla ya Sikukuu ya Krismasi, Disemba 25 mwaka 2020.

 

Kupitia kipengele cha Insta Story, Harmo aliwaposti warembo wakiongozwa na Wema Sepetu, Kajala, Irene Uwoya, Aunt Ezekiel, Hamisa Mobeto, Zuwena Mohamed ‘Shilole’, Jacqueline Wolper na Mimi Mars.

 

Gumzo likaanza hapo ambapo watu walijiongeza kwa kusema, kwa nini awaposti warembo hao na zaidi ilikuwa ni kwa Kajala ambaye tetesi zilikuwa zimezagaa kuwa ni mtuwe.

 

Baada ya madai ya Harmo na Kajala kusambaa kwa kasi, Kajala aliibuka na kukanusha kuwa hana ukaribu wowote wa kimapenzi na mkali huyo anayesumbua na wimbo wa Wapo.

 

Kajala alijitetea kuwa kama angekuwa karibu na Harmo asingeweza kumpeleka polisi kipindi fulani wakati msanii huyo alipomkosea.

 

Lakini pamoja na kanusho hilo, kwenye mkesha wa Mwaka Mpya, Harmo alionesha kwamba bado ‘hakomi’ kwani alimposti tena Kajala kwenye Insta Story na kusindikiza na maneno yalisosomeka: “My family.”

 

Licha ya wenyewe kutokiri suala la kuwa karibu kwa maana ya mahusiano ya kimapenzi, tetezi za kwamba wawili hao ni wapenzi zimekuwa zikiwaganda vibaya kupitia kurasa za wadaku huko Instagram.

Leave A Reply