The House of Favourite Newspapers

JESHI LA POLISI LAKAMATA SILAHA ZILIZOKUWA ZINATUMIWA NA WAHALIFU

Mkuu Wa Operesheni Maalum za Jeshi La Polisi, Naibu Kamishna wa Polisi (DCP) Liberates Sabas, akikagua na kuangalia silaha zilizokamatwa na askari Polisi katika operesheni maalum ya kutokomeza uhalifu nchini inayoendelea mkoani Mtwara.

Mkuu wa Operesheni Maalum za Jeshi la Polisi, Naibu Kamishna Liberates Sabas amesema Jeshi la Polisi kwa sasa linaendesha Operesheni mkoani Mtwara kwa kushirikiana na Nchi ya Msumbiji ili kuwakabili wahalifu wanaokimbili nchini humu.

Aidha  Jeshi la Polisi kupitia Operesheni Maalum inayoendelea mkoani Mtwara limefanikiwa kuwakamata watuhumiwa 96 kati yao 10 wamefikishwa mahakamani kwa kesi mbalimbali na  wengine 16 wamefikishwa katika idara ya Uhamiaji kwa makosa yanayohusu maswala ya uhamiaji katika operesheni hiyo kumepatikana siraha mbili zilizokuwa zikitumiwa na wahalifu katika maeneo mbalimbali.


Aidha Afande Sabas amewashukuru wananchi wa Mkoa wa Mtwara kwa kuendelea kutoa ushirikiano mzuri ndani ya Jeshi la Polisi na kuwataka wananchi wote nchini kuendelea kutoa ushirikiano ili kutokomeza uhalifu nchini.

 

Comments are closed.