The House of Favourite Newspapers

Rais Samia Aipongeza Marekani Mbele Ya Kamala Harris – “Serikali Yenu Ina Maana Sana Kwetu”-Video

0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan akutana na kuzungumza na Makamu wa Rais wa Marekani Kamala Harris, Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 30 Machi, 2023.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan akimpokea Kamala Harris, Makamu wa Rais wa Marekani Ikulu jijini Dar es Salaam na kuzungumza na vyombo vya habari leo Machi 30, 2023

KAMALA HARRIS: Marekani inaunga mkono kikamilifu ajenda ya Tanzania ya mageuzi ya kidemokrasia na ina dhamira thabiti ya kusaidia kuendeleza maadili ya kidemokrasia ya Tanzania.

Makamu wa Rais wa Marekani Kamala Harris akisaini Kitabu cha Wageni mara baada ya kuwasili Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 30 Machi, 2023. Pembeni yake ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu

Ziara ya Makamu wa Rais nchini Tanzania inathibitisha ubia huu imara baina ya nchi zetu mbili na itaimarisha zaidi ushirikiano katika biashara, jitihada za kutafuta ufumbuzi kuhusu usalama na uhakika wa chakula, ulinzi wa bayoanuai za majini, uwekezaji kwa wanawake na vijana, afya na kuimarisha demokrasia.

Katika kusaidia kuongeza wigo na kina cha uhusiano wetu rasmi, Serikali ya Marekani inakusudia kutoa Dola za Kimarekani milioni 560 kama msaada rasmi kwa Tanzania katika mwaka wa fedha wa 2024.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye mazungumzo na Mgeni wake Makamu wa Rais wa Marekani Kamala Harris mara baada ya kuwasili Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 30 Machi, 2023.

Hati ya Makubaliano itakayosainiwa kati ya Benki ya EXIM ya Marekani na Serikali ya Tanzania itapanua ushirikiano wa Kibiashara baina ya Marekani na Tanzania kwa kuziwezesha Kampuni za Kimarekani kuleta Nchini Tanzania bidhaa na Huduma bora za kibunifu

Makubaliano haya yatawezesha upatikanaji wa hadi Dola za Kimarekani milioni 500 kugharamia upelekaji wa Huduma na bidhaa katika sekta mbalimbali hususan, Miundombinu, Usafirishaji, Teknolojia ya Kidigitali, Nishati na Miradi ya Nishati jadidifu

Kuhusu Uendeshaji na Biashara ya Bandari, Marekani inalenga kusaidia jitihada za Serikali ya Tanzania kutumia kikamilifu fursa za uwekezaji na kuvutia wawekezaji wa aina mbalimbali, kulinda uwekezaji wake wa Kifedha na kuimarisha udhibiti wake wa Miundombinu hii muhimu kama Nchi huru

Leave A Reply