Mapokezi ya Magufuli Zanzibar ni Balaa! – Video
Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dkt. John Pombe ameshawasili Zanzibar leo, Ijumaa, Oktoba 2, 2020 akitokea Songwe na amepokelewa kwa nderemo na shangwe na wanachama wa CCM Visiwani humo.
Dkt. Magufuli amewasili Zanzinar kwa Ndege ya Watanzania Airbus (Twiga).
Kesho Oktoba 3, 2020 katika Viwanja vya Mnazi mmoja Zanzibar, Dkt. Magufuli atafanya Mkutano mkubwa wa Kampeni zake pamoja na kumuombea kura mgombea Urais wa Zanzibar kupitia CCM, dkt. Hussein Ali Hassan Mwinyi.