The House of Favourite Newspapers

Masha Love: Nioneni Tahira tu, Lakini…

0

UKIMUONA alivyo na wenge naamini utakuwa unajiuliza maswali mengi mno kichwani. Utajiuliza amekosa nini hadi anajiachia kiasi hicho. Kujichetua kwake kumepitiliza.

 

Hapa namzungumzia mwanamama Masha Love ambaye ametumia matiti yake kujitwalia umaarufu mkubwa ndani ya muda mfupi.

 

Wapo baadhi ya watu nje ya Bongo ambao wanaamini kabisa kwamba ni rahisi mno kupata umaarufu Bongo kuliko mahali pengine; ishu ni kuumiza tu kichwa utoke vipi.

 

Kupitia kurusharusha matiti, Masha Love amelamba madili makubwa na kupata fursa ya kwenda nchini Uturuki na huko ameendeleza vituko vyake hadi kuacha mshangao kwa wazungu.

 

Katikati ya mjadala mkali kuhusu Masha Love, Gazeti la IJUMAA limefanya naye mahojiano maalum kuhusiana na maisha yake na jinsi watu wanavyomchukulia na hapa anafunguka kila kitu;

 

IJUMAA: Habari yako Masha Love, hongera kwa shavu la Uturuki…

MASHA LOVE: Asante na ndiyo watajua hawajui kabisa, waache wanione tahira, lakini navuka nchi zote hivi karibuni na hao wanaoniona hivyo sidhani kama walishafika Ulaya.

IJUMAA: Kwa nini umesema kuwa wanakuona tahira?

 

MASHA LOVE: Unajua wengi wanaona mimi akili zimeruka, lakini baadaye watajiona wao ndiyo akili zimewaruka baada ya kuwaacha mbali sana kimaisha.

IJUMAA: Lakini Masha Love vipi kuhusiana na matiti yako, kwa nini uliamua kama ndiyo yawe biashara kwa upande wako?

 

MASHA LOVE: Ukweli ni kwamba matiti ndiyo yameongeza umaarufu wangu. Ni hivi; nimezaliwa na matiti makubwa na huko nyuma watu walikuwa wakinicheka sana, nikasema kuwa ipo siku hiki wanachonichekea kitakuwa faida kubwa kwangu, lakini hawakunielewa na leo hii matiti yangu ndiyo yamenileta Uturuki au Ulaya.

 

IJUMAA: Masha Love vipi kuhusu wazazi wako wanachukuliaje unavyojiachia?

 

MASHA LOVE: Kwanza naomba nikuambie wazi, wazazi wangu wote ni wafuasi wa Dini ya Kiislam, tena yenyewe kabisa na baba yangu ni shehe kabisa, lakini mwisho wa siku imebidi wakubali kwa sababu kila mtu anatafuta kazi kwa njia yake, maana mwisho wa siku wanaona mtoto wao ana viwanja, anamiliki gari, na ninawajali kwa mahitaji muhimu, ikabidi wavumilie tu na maisha mengine yaendelee.

 

IJUMAA: Hivi ni kweli katika ubalozi wa sabuni uliopata umelamba shilingi milioni 40 na nyumba umepata?

 

MASHA LOVE: Kweli kabisa, mimi mwenyewe mwanzo nilijua ni utani tu, lakini mara Napata visa, mara tiketi, maana niliwahi kupanda ndege mara moja tu nilivyokuwa nakwenda Tanga, lakini kupanda pipa kubwa siyo mchezo nakuambia kwa hiyo maisha yamebadilika na sabuni tunauza hatari, maana wengine walikuwa wananidharau kabisa, ila leo wameona kazi yangu.

 

IJUMAA: Vipi kuhusu uhusiano wako na Dokta Kumbuka maana najua ni mzazi mwenzako?

MASHA LOVE: Aende zake kule, hana sifa za kuwa baba yule, anashindwa kutoa hata pesa ya penseli ya mtoto wake, kazi kupiga domo bila sababu za msingi, sasa nimemzidi kwa kila kitu na asithubutu kuja anga zangu. Mtoto namlea kwa vile nina pesa ya kutosha sana kulea mwanangu.

 

IJUMAA: Vipi kuhusu kuolewa ndoa ya pili?

MASHA LOVE: Ni kweli kabisa, nimeolewa ndoa ya pili na nimetulia na ndoa yangu wala sina ugomvi na mke mwenzangu, tunakula vyetu kwa kutulia sana.

IJUMAA: Sasa ilikuwaje na shuka barabarani huko Uturuki?

 

MASHA LOVE: Ndiyo maana ya ubalozi, aibu ya nini na mara nyingi watu wanashindwa kabisa kufanya ubalozi kwa kujiona wao ndiyo wao siyo sawa kabisa, nimeitendea haki kazi niliyopewa.

IJUMAA: Ila Masha hivi karibuni ulikuwa Konde Gang, lakini sasa hivi naona umehamia WCB, hii imekaaje?

 

MASHA LOVE: Yaani ni hivi; wakae kwa kutulia, mimi ni WCB, kule kwingine nilikwenda kuganga njaa, ila kwa Diamond ndiyo kila kitu, maana hata nikiishiwa kodi naweza kusaidiwa, kule niliona kabisa nitakufa njaa.

IJUMAA: Poa Masha Love, shukurani sana.

MASHA: Asante sana Gazeti la IJUMAA na mimi nawapendajeee…

MAKALA: IMELDA MTEMA, BONGO

Leave A Reply