The House of Favourite Newspapers

Namungo Yalamba Milioni 635, Yatinga Makundi

0

LICHAya kwamba wawakilishi wa Tanzania kwenye Kombe la Shirikisho Afrika, Namungo FC, jana Alhamisi walipoteza mechi yao ya marudiano dhidi ya CD de Agosto ya Angola, lakini hilo haliwakuwazuia kufuzu hatua ya makundi ya kombe hilo.

 

Namungo FC waliandika rekodi hiyo ikiwa ni mara yao ya kwanza kufuzu hatua hiyo licha ya kuwa walipoteza mchezo huo uliochezwa kwenye Uwanja wa Azam Complex kwa mabao 3-1 lakini walifuzu kwa ushindi wa jumla wa mabao 7-5 na kuweka rekodi hiyo.

 

Bao pekee la Namungo FC kwenye mechi hiyo ya jana lilifungwa na kiungo mshambuliaji, Sixtus Sabilo huku ya Agosto yakifungwa na Brian Moya (mawili) na Natriano Da Costa.

Sasa Namungo wenye makazi yao mkoani Lindi wamefuzu makundi ambapo wamepangwa Kundi D na timu za Raja Casablanca ya Morocco, Nkana FC ya Zambia na Pyramid ya Misri, wakiwa pia wameshajihakikishai Sh milioni 635 kwa kufika hatua hiyo na wanaweza kupata zaidi kama watapata nafasi ya kusonga hatua zinazofuata.

 

Mchezo huo wa jana ulishuhudiwa na baadhi ya mashabiki wachache ambao waliruhusiwa kuingia uwanjani baada ya ule wa awali kushindwa kuingia kutokana na kuzuiwa na Agosto ambao ndiyo walikuwa wenyej

Leave A Reply