Rais Moi wa Kenya Yupo ICU
RAIS mstaafu wa Kenya, Daniel Arap Moi, mwenye umri wa miaka 95, yuko katika chumba cha wagonjwa wanaohitaji uangalizi maalumu (ICU) Hospitali ya Nairobi akipatiwa matibabu.
Hali ya afya wa Moi imekuwa ikitetereka kwani amekuwa akilazwa na kuruhusiwa hospitalini hapo mara nne tangu Oktoba 2019, akitibiwa tatizo la maji kujaa kwenye mapafu.
Moi aliyezaliwa Septemba 2, 1924 alikuwa ni rais wa pili wa Kenya na kuiongoza nchi hiyo kutoka mwaka 1978 hadi mwaka 2002.