Mbowe, Lema na Mbatia Wakicheza Blues (Pichaz + Video)
Joseph Haule ‘Profesa Jay’ amefunga ndoa na mchumba wake wa siku nyingi, Grace Mgonjo. Ndoa ya Prof Jay ambaye ni Mbunge Jimbo la Mikumi kupitia tiketi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), ilifungwa mchana wa Jumamosi, JULAI 08, 2017, katika Kanisa la Mtakatifu Joseph jijini Dar na usiku mpango mzima ulihamia kwenye Ukumbi wa Mlimani City jijini Dar ambapo mastaa wa muziki na filamu sambamba na wanasiasa, wengi wakiwa ni wabunge na viongozi wa Chadema walifurika.
Ulipofika muda wa kufungua muziki, Profesa Jay na mkewe walitia fora kwa kucheza ‘blues’ taratibu na kuwa kivutio kikubwa ukumbini hapo. Yote tisa, kumi ni pale waheshimiwa wabunge walipoanza kuyarudi, kila mtu na wake. Ilikuwa hapatoshi.
Profesa Jay, kabla ya ndoa hiyo, yeye na Grace wamejaliwa mtoto mmoja wa kike.
Shoo ya Diamond kwenye harusi hiyo ilibamba mno na kuwafanya wanakamati wawe na kazi ya ziada ya kutuliza watu watulie kwenye siti zao.
(PICHA: RICHARD BUKOS | GLOBAL PUBLISHERS)