The House of Favourite Newspapers

Waziri Mkuu wa Urusi Akutwa na Corona

0

WAZIRI Mkuu wa Russia Mikhail Mishustin amesema amekutwa na maambukizi ya virusi vya Corona.

Taarifa iliyotolewa na Makao Makuu ya Serikali ya Urusi imesema, Mishustin alimwambia rais wa nchi hiyo Vladmir Putin kwa njia ya video kuwa, amepimwa na kukutwa na virusi vya Corona.

Amesema amejitenga nyumbani kwake na kufuata maelekezo ya madaktari, na kuongeza kuwa, serikali itaendelea kufanya kazi kama kawaida.

Naibu wa kwanza wa Waziri Mkuu huyo Andrei Belousov atakaimu kwa muda kazi za waziri mkuu huyo, kufuatia hatua iliyoidhinishwa na rais Putin.

Leave A Reply