Wema Azua Mjadala “Napenda Kupigwa na Boyfriend Wangu”
Miss Tanzania 2006 na muigizaji wa muda mrefu nchini, @wemasepetu amedai aliwahi ahidiwa kutopigwa kwenye mahusiano kipindi anaanza mapenzi na mwanaume fulani ila hali ikabadilika na kiapo kikayeyuka🤪 akaanza kuchezea vitasa vya uhali gani mahabuba.👇
“Nakumbuka zamani wakati naanza mapenzi na mwanaume flani, alishanitamkia hajawahi na hatowahi kumpiga mwanamke… Ila kwangu bwana akagonga mwamba na hicho kiapo… Kiukweli nili enjoy sana…😂😂😂
Moral of the story: Kupigwa na baby wako kuna raha yake, haswa pale kwenye kubembelezana… Ila sasa sio tupigane kama wezi… Kidogo tu sio mbaya… Alafu iwe mara moja moja sio Daily… 😉😉😉
Sio lazima wote tufanane… Kuna wasio penda kupigwa ila as for me, kushtua shtua one tym is very Healthy jamani..” amesema Wema.