The House of Favourite Newspapers

Wolper Amtoa Harmonize kwa Wajuaji

Na Imelda Mtema | RISASI | HABARI FUPIFUPI

STAA wa filamu za Kibongo, Jacqueline Wolper kwa mara ya kwanza tangu aachane na mpenzi wake, Rajab Abdulhan ‘Harmonize’ ameibuka na kusema amewaachia penzi wajuaji.

Wolper alisema kuwa baada ya kumwagana na Harmonize kwa sasa ameamua kujikita zaidi katika kufanya mambo yake ya kimaendeleo na mambo ya mapenzi na msanii huyo wa Bongo Fleva amewaachia wajuaji ambao anaamini walikuwa wakimtolea macho kitambo.

“Harmonize nimewaachia wajuaji wawe naye, nimeamua kuwa bize na mambo yangu ya maendeleo zaidi, suala la mapenzi nimeliweka pembeni kwanza,” alisema Wolper.

Comments are closed.