The House of Favourite Newspapers

Mbunge wa CCM Amtembelea Lissu Hospitalini Nairobi

0
Tundu Lissu.

MBUNGE wa Singida Kaskazini, Lazaro Nyalandu (CCM) amemtembelea Mbunge wa Singida Mashariki na Mwanasheria Mkuu wa Chadema, Tundu Lissu aliylazwa katika Hospitali ya Nairobi nchini Kenya akitibiwa majeraha baada ya kushambuliwa kwa risasi wiki iliyopita nyumbani kwake, Area D, Dodoma.

Nyalandu ameandika;

“Nimefika Hospitali ya Nairobi mapema leo kumjulia hali Mh. Tundu Lissu. MADAKTARI wanaendelea kumfanyia matibabu, na bado hatujaruhusiwa kumuona.

“Kwa niaba ya Wana-Singida, na Watanzania wote, nimetoa salaam za pole kwa mke wake, na bado nasubiri uwezekano wa kuweza kuonana naye usiku wa leo endapo MADAKTARI wataruhusu.

“Cha muhimu zaidi, SOTE tuendelee KUMWOMBEA. MUNGU amtendee wema, na kumponya katika majira haya ya kujaribiwa kwake. Katika yote ndani ya yote, IKAWE HERI KWAKE. (Pichani na mdogowangu Peter Nyalandu, The Nairobi Hospital, Kenya).”

Nyalandu ameungana na Wabunge wa CHADEMA wakiwemo Freeman Mbowe, Godbless Lema, Joshua Nassary, Peter Msigwa na mbunge wa zamani Ezekiel Wenje, ambao nao wapo Nairobi kuangalia hali ya mgonjwa huyo.

Leave A Reply